Boost

Watu wengi walio na virusi vya hepatitisi hawatakuwa na dalili zozote mwanzoni. Unaweza kuwa na hepatitisi kwa miaka au hata miongo bila kufahamu. Lakini isipotibiwa, hepatitisi B na C zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya ini ikiwa ni pamoja na fibrosis (kovu la ini ambalo linaweza kutibiwa linapogunduliwa mapema), cirrhosis (aina ya uharibifu wa kudumu kwa muundo na utendaji wa ini) na saratani ya ini.

Baadhi ya dalili za mapema za onyo la homa ya ini ni pamoja na:
- uchovu
- kujisikia vibaya kwa ujumla
- matatizo ya tumbo na kupungua uzito
- homa ya nyongo ya manjano (ambapo ngozi au macho huwa ya rangi ya manjano)
- kichefuchefu
- mabadiliko ya rangi ya mkojo (kuwa nyeusi zaidi) au kinyesi (kuwa cheusi zaidi au cheupe zaidi)

Unaweza kuwa na baadhi ya dalili hizi na si zingine. Lakini hata bila dalili, maambukizi yanaweza kuharibu ini, kwa hivyo ni muhimu kupimwa ikiwa unafikiri unaweza kuwa katika hatari.

Neno 'hepatitisi' linamaanisha kuvimba kwa ini. Kwa hivyo, hepatitisi inaweza kuwa na visababishi kadhaa tofauti, ambavyo vyote husababisha kuvimba na uharibifu wa ini vikizuia kufanya kazi vizuri.

Hepatitisi inaweza kuwa matokeo ya chaguo fulani za mtindo wa maisha (pamoja na pombe nyingi na uvutaji sigara), sababu za kinjenetiki au maambukizi ya virusi. Hepatitisi nyingi duniani husababishwa na maambukizi ya virusi.

Kuna virusi 5 vikuu vya hepatitisi, ikiwa ni pamoja na:

Hepatitisi A: Hii huambukizwa kupitia chakula na maji ambayo yamekuwa yakitagusana na watu walio na virusi. Kuna chanjo ambayo inaweza kuzuia hepatitisi A.

Hepatitisi B: Hii huenea katika damu. Kwa kawaida huambukizwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Katika hali chache, inaweza kuambukizwa kupitia ngono na kushiriki vifaa vyenye ncha. Kuna chanjo ya kuzuia hepatitisi B.

Hepatitisi C: Hii kwa kawaida huambukizwa kupitia damu zinapokutana. Hepatitis C inaweza kutibiwa kwa dawa za kuzuia virusi.

Hepatitisi D: Hii huathiri tu watu ambao tayari wana hepatitisi B. Inaweza kuambukizwa kupitia damu zinapokutana au ngono. Hakuna chanjo ya hep D, lakini kupata chanjo ya hep B kutasaidia."Neno 'hepatitisi' linamaanisha kuvimba kwa ini. Kwa hivyo, hepatitisi inaweza kuwa na sababu kadhaa tofauti, ambazo zote husababisha kuvimba na uharibifu wa ini kuizuia kufanya kazi vizuri.

Hepatitisi inaweza kuwa matokeo ya chaguo fulani za mtindo wa maisha (pamoja na pombe nyingi na uvutaji sigara), sababu za maumbile au maambukizo ya virusi. Hepatitisi nyingi duniani husababishwa na maambukizi ya virusi.

Kuna virusi 5 vikuu vya hepatitisi, ikiwa ni pamoja na:

Hepatitisi A: Hii huambukizwa kupitia chakula na maji ambayo yamekuwa yakitagusana na watu walio na virusi. Kuna chanjo ambayo inaweza kuzuia hepatitisi A.

Hepatitisi B: Hii huenea katika damu. Kwa kawaida huambukizwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Katika hali chache, inaweza kuambukizwa kupitia ngono na vifaa vyenye ncha. Kuna chanjo ya kuzuia hepatitisi B.

Hepatitisi C: Hii kwa kawaida huambukizwa kupitia damu zinapokutana. Hepatitis C inaweza kutibiwa na dawa za kuzuia virusi.

Hepatitisi D: Hii inaathiri tu watu ambao tayari wana hepatitisi B. Inaweza kuambukizwa kupitia damu zinapokutana au ngono. Hakuna chanjo ya hep D, lakini kupata chanjo ya hep B kutasaidia.

Hepatitisi E: Hii inahusishwa na kula nyama ya nguruwe au samakigamba isiyopikwa ikaiva inavyofaa. Kwa kawaida ni maambukizi madogo na ya muda mfupi lakini yanaweza kuwa mabaya zaidi kwa watu walio na mifumo dhaifu ya kinga.      

 

Ikiwa unaweza kuwa katika hatari ya kupata hep B au hep C, ni muhimu kupimwa. Baada ya kufahamu kuwa una virusi unaweza kupata matibabu. Hii itakusaidia kuwa na afya na kuzuia ini lako kuharibika katika siku zijazo.

Hep B:
Kipimo cha damu kinaweza kutafuta antijeni za hep B (sehemu za virusi vyenyewe). Kipimo hiki kinaweza kuonyesha ikiwa una hep B kuanzia wiki ya 6 hadi ya 12 baada ya kuambukizwa. Katika hali nyingi, hep B inaweza kuondolewa kutoka katika mwili bila matibabu, haswa ikiwa ulipata chanjo ya hep B. Hata hivyo, kwa watu wengine, maambukizi yatahitaji kutibiwa ili kuzuia uharibifu wa ini.

Hep C:
Kipimo cha damu kitapima kingamwili za hep C. Hizi ni sehemu za mfumo wako wa kinga na zitaonyesha ikiwa mwili wako umegusana na virusi vya hep C. Matokeo chanya ya kipimo cha kingamwili yanaweza kumaanisha kuwa una virusi sasa au kwamba umewahi kuwa na virusi hapo awali. Ili kujua ikiwa una hep C sasa, vipimo chanya vya kingamwili vitahitaji kufuatwa na 'vipimo vya virusi vya PCR'. Watu walio na VVU wanaweza kupimwa kiwango cha virusi kwanza, kwa sababu vipimo vya kingamwili vinaweza kuwa sahihi kidogo. Hepatitisi C inaweza kutibiwa kwa matibabu ya moja kwa moja ya kupambana na virusi.