Boost

Chawa wa kwenye sehemu za siri (pia hujulikana kama kaa au ukurutu) ni wadudu wadogo ambao hupatikana kwenye nywele za mwilini, kama vile mavuzi, nywele za kwapani na mara kwa mara kwenye ndevu. Hawaishi katika nywele za kichwani.

Wanaweza kusambazwa kupitia mgusano wa karibu wa mwili, kwa mfano kupitia ngono. Kutumia kondomu hakuwezi kukuzuia kupata chawa wa sehemu za siri. Jambo bora la kufanya ni kumwona mhudumu wa afya ikiwa unafikiri una dalili. Dalili kuu ni kuwashwa katika eneo lililoathirika, hasa wakati wa usiku. Unaweza pia kubaini mwako fulani unaosababishwa na kukuna, unga mweusi katika nguo yako ya ndani na madoa ya bluu au madoa madogo ya damu kwenye ngozi yako.

Ili kujua ikiwa una chawa wa kwenye sehemu za siri mhudumu wa afya atakufanyia vipimo. Mara baada ya kugundulika unaweza kutibu chawa wa sehemu za siri kwa kutumia malai ya kuua wadudu, losheni au shampuu.  

Ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili ni maambukizi yanayosababishwa na kuvu ya chachu. Inaweza kuathiri uke, uume, mdomo na katika hali nadra zaidi maeneo mengine ya mwili. Hauchukuliwi kama ugonjwa wa maambukizi ya zinaa, lakini unaweza kusababishwa na ngono na wakati mwingine kuambukizwa kupitia ngono, ingawa hii si jinsi watu wengi wanavyoupata.

Ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili ni wa kawaida sana na kwa kawaida hauna madhara. Inakadiriwa kuwa wanawake 3 kati ya 4 watakuwa na ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili wakati fulani maishani mwao. Wanaume pia wanaweza kupata ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili, lakini huwa si kawaida. Mara nyingi watu hawatagundua dalili zozote, lakini inaweza kusababisha kutokwa na uchafu mweupe kwenye uume ua uke wako, kuhisi kuwashwa pamoja na kujisikia kuchomeka karibu na sehemu za siri.. Kwa kuwa hizi ni dalili za kawaida kwa magonjwa mengine ya zinaa pia, ni muhimu kumwona mtoa huduma wa afya ikiwa utagundua dalili hizi.

Una uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili ikiwa:
1. unavaa mavazi yaliyobana
2. unatumia sabuni au bidhaa nyingine kwenye uke wako
3. una kisukari, VVU au magonjwa mengine yanayoathiri mfumo wako wa kinga.

Ugonjwa wa kuvimba ndani ya mwili hutibiwa kwa urahisi kwa dawa za kuzuia kuvu.

Maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ni maambukizi yanayotokea kwenye mrija wa urethra, mshipa unaotumika kutoa mkojo nje. Ugonjwa huu ni wa kawaida zaidi kwa wanawake kuliko wanaume kwa sababu wanawake wana mrija mfupi wa urethra. Hauambukizwi kwa njia ya ngono na si ugonjwa wa kuambukiza. Ingawa, wanawake mara nyingi wanaweza kupata UTI baada ya ngono. Hii ni kwa sababu bakteria wanaweza kuingia kwenye mrija wa urethra wakati wa ngono.

Ili kuepuka kupata UTI, ni vyema kukojoa kabla na baada ya kufanya ngono. Unapaswa pia kuepuka kufanya vitu ambavyo vinaweza kuhamisha bakteria kutoka kwenye sehemu ya haja kubwa kwenda kwenye uke na mrija wa urethra, kwa mfano kuhama kutoka kwenye ngono ya njia ya haja kubwa kwenda kwenye uke. Ukifanya hivi, unapaswa kutumia kondomu mpya kwa ngono ya ukeni. Pia ni vyema kunawa mikono yako kabla ya kugusa sehemu za siri za mwenzi wako.

katika hali za maaumbukizi ya UTI mara nyigi huwa inapona enyewe bila  matibabu maalum. Jaribu kunywa maji mengi na usiuzuie mkojo wako. Ikiwa maambukizi yatadumu kwa zaidi ya siku 4, unapaswa kuzungumza na mhudumu wa afya. Pia ni vyema kuzungumza na mhudumu wa afya ikiwa hujawahi kupata UTI hapo awali, kwani wakati mwingine dalili zinaweza kuwa zinafanana na magonjwa ya zinaa. Wanaweza pia kukupatia viua vijasumu ili kutibu maambukizi ikiwa inahitajika.